Pages

Followers

Powered by Blogger.

Tuesday, 4 June 2013

ABSALOM KIBANDA AREJEA TOKA KWENYE MATIBABU SA


1Mhariri Mtendaji wa kampuni ya New Habari Absalom Kibanda amerejea leo nchini baada ya kupata matibabu yake nchini Afrika Kusini ambako alipelekwa baada ya kujeruhiwa na watu wasiojulikana tangu mwezi wa tatu mwaka huu, Absalom Kibanda amepokelewa na wahariri, Waandishi wa habari na watu mbalimbali kwenye uwanja wa ndege wa J.K.Nyerere ambapo aliwasili ndege ya kwa shirika la ndege la Afrika Kusini SA, Crew ya Fullshangwe inakupa pole lakini pia tunaomba mungu akupe nguvu na  ujasiri zaidi kwani wewe ni mja wake

MWILI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEA WAWASILI NCHINI TAYARI KWA MAZISHI

Monday, 20 May 2013

TAZAMA MAANDAMANO MBUNGE MSIGWA ALIPOACHIWA KWA DHAMANA



  Wafuasi  wa Chadema Iringa  wakiwa  wamembeba  juu juu mbunge  wa  jimbo  la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa  baada ya  kuachiwa kwa  dhamana  leo hadi kesi  hiyo itakapotajwa tena Juni 3 mwaka  huu  huku wafuasi  wake  26 kati ya 74 wakosa 

Thursday, 9 May 2013

RAIS KIKWETE AIAGA BATALIONI ITAYOJIUNGA NA MAJESHI YA UMOJA WA MATAIFA YA KULINDA AMANI DRC


jw1Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi bendera kiongozi wa batalioni ya  wanajeshi wa JWTZ wanaokwenda kujiunga na  jeshi la Umoja wa Mataifa la kulinda amani Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, katika sherehe za kuwaaga zilizofanyika Msangani, Kibaha, Mkoa wa Pwani leo Mei 8, 2013. Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Shamsi Vuai Nahodha na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange wanashuhudia.

WABUNGE WATAKA UMOJA KULINDA AMANI, WACHOCHEZI KUDHIBITIWA


wabunge
NA  MAGRETH KINABO – MAELEZO, DODOMA
 BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   limeazimia kuitaka Serikali kuchukua mara moja dhidi ya viashara  vya aina yoyote ya uvunjifu wa amani unaojitokeza  ilikuwapa wananchi  matumaini ya kujumuika na kubudu kwa uhuru bila kuwa na hofu ya usalama wao.
 Azimio hilo limepitishwa leo Bungeni kufuatia Mwenyekiti wa  Kamati ya  Bunge ya Ulinzi na Usalama, Anna Abdallah  alipowasilisha Azimio la Bunge la Kulaani Tukio la Kulipuliwa kwa Bomu katika Kanisa la Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olasiti, jijini Arusha , Mei 5,mwaka huu.

Wednesday, 8 May 2013

CHUO CHA KIU-DCC KUSIMAMISHWA KUTOA MAFUNZO YA SHAHADA ZA UZAMILI NA UZAMIVU


Kampala International University, Kampasi ya Dar-es-Salaam (KIU-DCC) kilichopo Gongo la Mboto, Dar-Es-Salaam ni Chuo kilichopewa idhibati na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU). Kufuatia kuendesha mafunzo ya shahada ya Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) kinyume cha utaratibu na kutokua na wahadhiri wa kutosha wenye sifa stahili, Tume katika mkutano wake wa hivi karibuni ulikiamuru Kampala International University, Kampasi ya Dar-es-Salaam ifuatayo;

MH. PINDA AWAFARIJI WALIOJERUHIWA KWENYE TUKIO LA BOMU JIJINI ARUSHA


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapa pole baadhi ya majeruhi wa bomu la kutupwa kwa mkono lililolipuka katika kanisa Katoliki la Olasiti Arusha wakati alipowatembelea kwenye hospitali ya mkoa wa wa Arusha, Mount Meru, May 8,2013.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).